Mwenza huyu simtaki, yu bado ang’ang’ania,
tena eti kahamaki, , hataki niachilia
Kama vile sina haki, kwa ninacho hitajia
Kajawa na taharuki, haki yangu kuijua
tena eti kahamaki, , hataki niachilia
Kama vile sina haki, kwa ninacho hitajia
Kajawa na taharuki, haki yangu kuijua
Mwanzo nilimrizia, kwa alivyo nidanganya
Sejua wake uzia, udugu kuuchanganya
sekuwa nikisinzia, hadaze zenikanganya
Hadi kuja nitanzia, alilotaka kufanya
Sejua wake uzia, udugu kuuchanganya
sekuwa nikisinzia, hadaze zenikanganya
Hadi kuja nitanzia, alilotaka kufanya
Silaumu wangu baba, ambae kanipeleka
Hakufanya kisiriba, wasia aliuweka
He sema akinikaba, naweza kumuepuka
Ila naona msiba, amezidi kunishika
Hakufanya kisiriba, wasia aliuweka
He sema akinikaba, naweza kumuepuka
Ila naona msiba, amezidi kunishika
Ananivuta mashati, kila nikipapatuwa
Kuvuta hewa sipati, nihitajipo pumuwa
Tena ana tashititi, kejeli kajaaliwa
Kaniwekesha shariti, yutayari kuniuwa
Kuvuta hewa sipati, nihitajipo pumuwa
Tena ana tashititi, kejeli kajaaliwa
Kaniwekesha shariti, yutayari kuniuwa
(Mzalendo.net)
1 maoni:
bora umtoroke
Chapisha Maoni