Matini Muhimu :
Home » , » MOHAMED SAID ABDULLA (Bwana. MSA) BABA WA RIWAYA PENDWA

MOHAMED SAID ABDULLA (Bwana. MSA) BABA WA RIWAYA PENDWA

Imeandikwa na; Unknown mnamo, Jumanne, 17 Desemba 2013 | Jumanne, Desemba 17, 2013



Mohamed Said Abdulla alizaliwa mnamo mwaka 1918 katika mtaa wa Malindi Zanzibar. Alipelekwa chuoni ambako alijifunza kusoma Kurani. Mwaka 1928 alisoma masomo ya msingi katika shule ya serikali. Alifanikiwa kuendelea na masomo ya sekondari mwaka 1938 katika shule ya serikali pia. Baada ya kuhitimu aliajiriwa kuwa ofisa wa afya ambako alifanya kazi hiyo mpaka mwaka 1958 wakati ajira yake ilipokatishwa. Baada ya kuachishwa kazi katika idara ya afya alifanikiwa kupata ajira nyingine katika gazeti la Mkulima kama mhariri. Alifanya kazi hiyo hadi mwaka 1968 pale alipoachishwa tena kazi ya uhariri katika gazeti hilo. Baada ya kuachishwa kazi hiyo alipata kazi ya utayarishaji kipindi cha redio kilichoitwa Sadiki Ukipenda katika Sauti ya Unguja. Katika uhai wake alioa na kupata watoto wanne.

Katika taaluma ya fasihi mchango wake unaonekana sana katika taaluma ya riwaya kwani aliandika na kuchapisha riwaya saba pamoja na hadithi fupi moja kama ifuatavyo;

Mzimu wa Watu wa Kale ,Kisima cha Giningi, Duniani kuna watu, Siri ya Sifuri, Mke Mmoja Waume Watatu, Mwana wa Yungi Hulewa, Kosa la Bwana Msa, Mke Wangu ambayo ni hadithi fupi. Mohamed Said Abdulla alifariki mnamo mwaka 1992. Historia hii ni kwa mujibu wa (BAKIZA 2007)
Sambaza hii :

0 maoni:

Tafuta Kwenye Wikipedia

Matokeo ya utafutaji

 
Kwa Hisani ya : Muunda Blogu | Nawaje Ali | NAM
Fahari kwa Kiswahili Jukwaani
Hakimiliki © 2013 - 2018. Kiswahili Jukwaani - Haki Zote Zimehifadhiwa