Matini Muhimu :
Home » » KATIBA YA CHAWAKAMA

KATIBA YA CHAWAKAMA

Imeandikwa na; Unknown mnamo, Jumatano, 1 Januari 2014 | Jumatano, Januari 01, 2014

                                 


CHAMA CHA WANAFUNZI WA KISWAHILI VYUO VIKUU 
AFRIKA MASHARIKI (CHAWAKAMA). 




 KATIBA YA AFRIKA MASHARIKI.


                                         



Tovuti: www.chawakama-am-webs.com 
Barua pepe: chawakama2004@yahoo.com 



“KISWAHILI HAZINA YA AFRIKA KWA MAENDELEO ENDELEVU” 
                                   .
CHAMA CHA WANAFUNZI WA KISWAHILI VYUO VIKUU 
AFRIKA MASHARIKI (CHAWAKAMA). 



YALIYOMO:

SEHEMU YA KWANZA                                                                       UKURASA    
   1.1. JINA LA CHAMA……………………………………………………… 2
   1.2. WALEZI WA CHAMA………………………………………………… 2
SEHEMU YA PILI            
                     2.0. MALENGO  NA  MADHUMUNI YA CHAMA………………………2              
SEHEMU YA TATU    
    3.0. UANACHAMA NA ADA……………………………………… ………3
    3.1. AINA ZA UANACHAMA…………………………………………….  3
    3.2. HAKI ZA MWANACHAMA…………………………………………. 3
    3.3. KIINGILIO NA ADA YA MWAKA………………………………….  4
    3.4. KUSITA UANACHAMA………………………………………………4
    3.5. WAJIBU WA MWANACHAMA……………………………………...4

SEHEMU YA NNE.
4.1. MUUNDO WA UONGOZI.. ...…………………………………………... 5
4.2. MUDA WA UONGOZI……………………………………………...……5
4.3. MASHARTI YA UONGOZI………………………………………...……5
4.5. WAJIBU WA VIONGOZI…..…………………………………………….6
SEHEMU YA TANO.
5.0. FEDHA ZA CHAMA…………………………………………………….. 7
5.1. VYANZO VYA MAPATO………………………………………………..7
5.2. UWEKAJI, UCHUKUAJI WA FEDHA……………………….………….7
SEHEMU YA SITA.
6.0. VIKAO VYA CHAMA ………………………………………………….. 8
                   6.1. VIKAO VYA KAMATI KUU…………………………………………… 8
6.2. VIKAO VYA KAMATI YA UTENDAJI………………………………………..8
6.3. VIKAO VYA KAMATI YA NIDHAMU NA USIMAMIZI……………………9
6.4. MKUTANO MKUU WA CHAMA………………………………………………9

SEHEMU YA SABA
7.1.MABADILIKO YA KATIBA…………………………………………………….10
7.2. MRITHI WA CHAMA………………………………………………………...…10



                                   .
CHAMA CHA WANAFUNZI WA KISWAHILI VYUO VIKUU
AFRIKA MASHARIKI (CHAWAKAMA).

                                     
SEHEMU YA KWANZA


1.1.  JINA LA CHAMA

Jina la chama ni CHAMA CHA WANAFUNZI WA KISWAHILI
VYUO VIKUU VYA AFRIKA MASHARIKI, Kwa kifupi-(CHAWAKAMA)

            Makao makuu  ni Chuo Kikuu cha Waislamu cha Morogoro
(MUM).

1.2.   WALEZI WA CHAMA
                 Walezi wa  chama katika Afrika mashariki.
 
1.2.1  Taasisi ya Taaluma za Kiswahili (TATAKI)-TANZANIA.
1.2.2                                                                         KENYA.
1.2.3                                                                         UGANDA.
1.2.4                                                                         RWANDA.
1.2.5                                                                         BURUNDI.

                                                     
                                                     















                                   .

SEHEMU YA PILI.

            20.    MADHUMUNI YA CHAMA.
          2.1.   Kuwapa wanachama nafasi ya kujadili, kuimarisha, na kukuza vipawa
                   vyao
2.1  Kuamsha ari ya mapinduzi ya utamaduni wa lugha ya Kiswahili
2.2  kueneza lugha ya Kiswahili ndani na nje ya Afrika Mashariki.
2.3  kushirikiana na vyama vingine vya Kiswahili katika juhudi ya kuendeleza
na kuimarisha lugha ya Kiswahili ndani na nje ya Afrika Mashariki.
2.4  Kuunganisha wanafunzi wa lugha ya Kiswahili katika vyuo vikuu vya
ndani na nje ya Afrika Mashariki.
2.5  Kushirikiana na Asasi mbalimbali zinazojihusisha na ukuzaji na uenezaji
wa Kiswahili Afrika Mashariki na Afrika yote kwa ujumla.
2.6  .Kuratibu makongamano ya mijadala mbalimbali inayohusu lugha ya
Kiswahili.
2.7  Kuchapisha jarida la CHAWAKAMA na machapisho mengine ili kukuza
taaluma ya Kiswahili.
2.8     Kubuni mikakati na mbinu za kuhimiza ukuzaji na uenezaji wa lugha ya
Kiswahili.
2.9  Kuweka kumbukumbu ya wataalamu kwa nia ya kuwatumia  katika
kufanikisha malengo ya Chama na wahusika wa Kiswahili kwa ujumla.

   
SEHEMU YA TATU
3. UANACHAMA NA ADA.
Uko  huru  kwa  mtu  yeyote  anayependa  kujiunga  na  kutekeleza  mambo  yote
yanayohusiana  na  Chama  kama  kulipa kiingilio  na ada, kuhudhuria vikao  na
kushiriki katika kazi za  kuiendeleza lugha ya Kiswahili.
Wanaoomba kujiunga na chama sharti wawe mwaka wa kwanza kwa shahada
ya uzamili.
Wanachama  watakaojiunga  mwaka  wa  tatu  wa  masomo  yao  watalipa  ada  ya
miaka yote mitatu iliyopita.
         
3.1      AINA ZA UANACHAMA
3.1.1.   Uanachama wa kawaida.
                                   .
           (a) Wanachama waliochuoni.
           Unawahusu Wanafunzi wote wanaosoma somo la Kiswahili katika Vyuo
           Vikuu Afrika Masharikikwa kiwango cha shahada ya awali na shahada
           Ya uzamili.
           (b) Wanafunzi wasiosoma Kiswahili walio wazalendo wa lugha Kiswahili
           Walioko Vyuo Vikuu Afrika Mashariki.

3.1.1.1.Wanachama walio Chuoni.
Unawahusu  wanafunzi  wote  wanaosoma  somo  la  Kiswahili  katika  Vyuo      
Vikuu  vya    Afrika  Mashariki  katika  kiwango  cha  shahada  ya  kwanza  na
shahada  za Uzamili.

3.1.1.2 Wanachama nje ya Chuo.
Unawahusu wote walio nje ya Chuo na waliohitimu masomo wakiwa  
wanachama wa CHAWAKAMA.
             Iwapo ataomba uanachama kwa kujaza fomu maalumu kutoka katika matawi                
ya chama yaliyo hai.

3.1.2  Wanachama washiriki
              Asasi zinazoshughulikia ukuzaji na uenezaji wa Kiswahili zinaweza  
kukubaliwa kuwa mwa anachama baada ya kuwasilisha maombi na
kukubaliwa na kamati ya utendaji ya Chama kwa kutimiza masharti
yatakayotolewa.
     
3.1.3  Uanachama wa Heshima
Hawa ni watu au taasisi ambazo kwa mchango maalumu wameonekana au
zimeonekana zinafaa Kupewa uanachama wa Heshima.

3.1.4  Uanachama wa wadhifa
        Unawahusu walezi na wanataalamu wa somo la Kiswahili.

3.1.5  HAKI ZA MWANACHAMA.
Wanachama wote isipokuwa Wanachama Washiriki, Wanachama wa Heshima
na Wanachama wa Wadhifa watakuwa na haki zifuatazo:
3.1.5.1 .kupiga kura wakati  wa uchaguzi.
3.1.5.2 . kugombea nafasi ya uongozi katika Chama kwa mujibu  wa katiba hii.
3.1.5.3 .kuwasilisha hoja kwa ajili ya kujadiliwa katika Mkutano Mkuu.
                                   .
 
3.3.0.  KIINGILIO NA ADA.
3.3.1  Kila mwanachama atalipa kiingilio ambacho kitapangwa na Kamati ya Utendaji
na kuthibitishwa na Mkutano Mkuu.
3.3.2  Kila  mwanachama atatakiwa kutoa ada ya mwaka, kiasi ambacho kitapangwa
na kamati ya Utendaji na kuthibitishwa na Mkutano Mkuu.
3.3.3  Fedha zote katika kipengele(3.3.1) hapo juu  zitakuwa katika mgawanyo
ufuatao:
Asilimia 30 itakwenda Afrika Mashariki, Asilimia 30 itakwenda Kanda na
Asilimia 40 itabaki tawini. Viwango hivi vitakuwa vikibadilika kulingana na
wakati.

3.4  KUSITA UANACHAMA.
        Uanachama utasita kwa sababu zifuatazo:
3.4.1  Kutohudhuria mikutano ya chama mara tatu mfululizo bila ya taarifa na sababu
za kuridhisha.
3.4.2  Kutolipa ada  ya mwaka kwa muda wa miaka miwili mfululizo.
3.4.3  Kujiuzulu uanachama.
3.4.4  Kufukuzwa au kuachishwa uanachama na Mkutano Mkuu kwa kura
zisizopungua robo tatu ya wajumbe waliohudhuria.
3.4.5  Kifo cha mwanachama.
3.4.6  Kutokuwa katika hali  ya akili timamu.

 3.5.0  WAJIBU WA MWANACHAMA
 3.5.1  Kueneza na kukuza lugha ya Kiswahili.
 3.5.2  Kulipa ada na michango mingine
        3.5.3  Kutoa maoni juu ya mwenendo wa chama ili kukiimarisha chama.
        3.5.4  Kukuza kipaji chake kwa kupitia majarida na makala mbalimbali
        3.5.5  Kugombea nafasi za uongozi.
        3.5.6  Kuchagua viongozi
        3.5.7  Kuhudhuria vikao vya chama

 
SEHEMU YA NNE.

4.1     UONGOZI
4.1.1  CHAWAKAMA Afrika  Mashariki Viongozi  watakuwa:
                                   .
Mwenyekiti, Makamu  Mwenyekiti,Katibu Mkuu, Naibu Katibu, Mweka
Hazina, Mweka Hazina Msaidizi, Afisa Uhusiano, Afisa uenezi, Mhariri
Mkuu na Mhariri Msaidizi.

4.1.2   Viongozi wa CHAWAKAMA Afrika mashariki watachaguliwa  kulingana
na mgawanyo wa nafasi za uongozi, na watapitishwa na Mkutano Mkuu wa
chama wa Afrika Mashariki.

4.1.3  Kwa kadri inavyowezekana nafasi za uongozi wa Chama zitagawanywa
sawa kwa Kanda na matawi husika katika Kanda isipokuwa Katibu Mkuu
atatoka  yalipo Makao Makuu ya Afrika Mashariki.

4.1.4  Wenyeviti na makatibu wa kanda ni wajumbe wa kamati ya utendaji ya
Afrika Mashariki.

4.1.5  Kutakuwa na kamati ya Nidhamu na Usimamaizi ya Afrika mashariki.
(kamati itakuwa na Mwenyekiti na Katibu)

4.1.6  Kamati ya Nidhamu na Usimamizi wa kanda itaundwa na wajumbe watano
ambao watateuliwa na kamati ya utendaji ya kanda  husika katika  kikao cha
kwanza.


4.2   MUDA WA UONGOZI.
 4.2.1 Kamati ya Utendaji itakuwa madarakani kwa muda wa mwaka mmoja,Wajumbe  wa          
        Kamati wanaweza kuchaguliwa tena kwa kipindi kingine kisichozidi miaka miwili  
       isipokuwa Mwenyekiti, Katibu Mkuu na Mhazini ambao wataongoza kwa mwaka
mmoja tu na nafasi zao kupokelewa na Makamu au Manaibu wao.
     
4.2.2  kamati ya Nidhamu na usimamizi itakuwa madarakani kwa muda wa miaka mitatu  
       tangu tarehe ya uteuzi.


4.3    MASHARTI YA VIONGOZI.
     Kiongozi anatakiwa:
i.  Kuwajibika kwa mujibu wa Katiba.
ii.  Kuhudhuria vikao vyote vya Chama.
iii.  Kutunza mali na hadhi ya Chama.
iv.  Kutotoa na kupokea  rushwa.
v.  Kujiuzulu anapoona kazi imemshinda.
                                   .
vi.  Kukubali kuwajibika.

4.4   WAJIBU WA VIONGOZI.

4.4.1  Mwenyekiti.
i.  Msimamizi  mkuu wa shughuli za Chama.
ii.  Msemaji  mkuu wa  Chama.
iii.  Mwongoza mikutano ya Chama (Kamati Kuu na Mkutano Mkuu)
iv.  Kiongozi wa misafara ya Chama.
v.  Kusimamia nidhamu ya viongozi.

4.4.2   Makamu wa Mwenyekiti.
i.  Msaidizi  Mkuu wa  Mwenyekiti.
ii.  Mwenyekiti wa vikao vyote vya Chama kama Mwenyekiti hayupo.
iii.  Msaidizi na Mshauri wa  Mwenyekiti.
iv.  Kufanya kazi nyingine atakazoagizwa na Mwenyekiti.

4.4.3   Katibu Mkuu.
i.  Mtendaji Mkuu wa Chama.
ii.  Mtunza kumbukumbu za Chama.
iii.  Mtunza mali ya Chama.
iv.  Katibu wa mikutano ya Chama.
v.  Kuitisha vikao.
vi.  kuidhinisha matumizi ya fedha za Chama.
vii.  Kuratibu shughuli za Chama.
viii.  Kutoa ripoti juu ya maendeleo ya Chama.
ix.  Kutunza orodha ya wanaChama.
x.  Kutunza mihuri ya Chama.

4.4.4  Katibu Msaidizi.
i.  Msaidizi wa Katibu Mkuu
ii.  Mshauri wa Katibu Mkuu
iii.  Kufanya kazi zote za Katibu Mkuu wakati hayupo
iv.  Kufanya kazi nyingine atakazoagizwa na Katibu Mkuu

4.4.5  Mweka Hazina.
i.  Atakuwa  mdhibiti mkuu wa fedha na mali za Chama.
                                   .
ii.  Atahakikisha kuwa kuna mfumo mzuri wa kupokea, kudhibiti na kulipa fedha
za Chama.
iii.  Atatengeneza makisio ya mapato na matumizi ya Chama
iv.  Atafanya malipo kwa kufuata taratibu na kanuni za fedha zilizowekwa
v.  \Atakuwa mweka saini wa lazima katika akaunti za benki za Chama
vi.  \Ataandika na kutunza vitabu vya hesabu ya Chama
vii.  \Atatayarisha hesabu  na taarifa  za  fedha za mwaka  na kuziwasilisha kwa
kamati ya utendaji kabla ya kuwasilisha katika Mkutano Mkuu .
viii.  Atatunza  na kudhibiti mali na raslimali za Chama
ix.  Atahakikisha kuwa kila mwisho wa mwaka wa fedha, mali yote inahakikiwa.

4.4.6 Mweka Hazina Msaidizi.
i.  Atamsaidia mweka  hazina  kudhibiti fedha na mali za Chama
ii.  Kusaidia kuhakikisha kuwa kuna mfumo mzuri wa kupokea, kudhibiti na
kulipa fedha za Chama.
iii.  Kusaidia kutengeneza makisio ya mapato na matumizi ya Chama
iv.  Kusaidia kufanya malipo kwa kufuata taratibu na kanuni za fedha
zilizowekwa
v.  Atafanya kazi zote atakazoagizwa na Mweka Hazina Mkuu pamoja na
Mwenyekiti.

4.4.7  Afisa Uhusiano.
i.  Atabuni na kuratibu mipango ya ushirikiano miongoni mwa nchi na asasi
wanachama
ii.  Kutembelea asasi wanachama ili kufuatilia shughuli za Chama
iii.  Katika utekelezaji wa majukumu haya, Afisa uhusiano atashirikiana kwa karibu na
Katibu na Makamu Mwenyekiti, Naibu katibu, na Mhariri Mkuu.

4.4.8  Afisa Mwenezi.
         Atasimamia utangazaji na uenezi wa shughuli za Chama ili kuleta mahusiano mema
na  maelewano  na  umma,  Vyombo  vya  Habari,  Serikali,  Mashirika  ya  uhisani  na
asasi nyinginezo.

4.4.9  Mhariri Mkuu.
i.  Atasimamia na kuratibu uandaaji, uhariri na utoaji wa jarida la Chama
pamoja na vitabu., Machapisho hayo yanaweza kuwa katika umbo la
karatasi au la elektroniki.
ii.  Atakuwa ndiye mratibu mkuu wa masuala ya ushirikiano katika uchapishaji
na ubadilishaji wa machapisho.

                                   .
       
5.0    Kamati ya Nidhamu na Usimamizi.
i.  Itasimamia nidhamu ya viongozi wote wa kanda .
ii.  Itapokea na kushughulikia matatizo/migogoro itakayojitokeza ndani ya
uongozi kwa  kushirikiana na Mlezi wa Chama.
iii.  Itashirikiana na Uongozi juu ya uendelezaji wa shughuli za chama.



SEHEMU YA TANO

5.1     FEDHA ZA CHAMA
 5.1.1   Vyanzo vya mapato
               
               Mapato ya Chama ni;
5.1.2  Kiiingilio na Ada ya mwaka ya kila mwanaChama

5.1.3  Misaada, zawadi au ruzuku kutoka kwa wafadhili, wanachama, wahisani, watu
binafsi na vyombo vingine.

5.1.4  Mapato yatokanayo na shughuli mbalimbali au miradi ya Chama

5.1.5  Fedha itokanayo na  mikopo

5.1.6  Mwanachama au mfadhili yeyote wa Chama anaweza kutoa fedha au kukisaidia
Chama kwa njia yoyote atakayoona inafaa.

5.2  Uwekaji, uchukuaji wa fedha za chama.
   
5.2.1    Fedha za Chama zitawekwa katika benki itakayoteuliwa na Kamati ya
Utendaji.

5.2.2     Kutafunguliwa akaunti mbili katika benki;
5.2.2.1  Akaunti ya matumizi ya kawaida
5.2.2.2  Akaunti ya mfuko wa maendeleo wa ukuzaji na uenezi wa  
                   lugha.

                                   .
5.2.3   Watia saini
5.2.3.1  Mwenyekiti wa Afrika Mashariki
 
5.2.3.2  Katibu wa Afrika Mashariki

5.2.3.3   Mhazini wa Afrika Mashariki

5.2.3.4  Katibu wa kamati ya Nidhamu na Usimamizi ya Afrika Mashariki.
                Kamati Kuu itaandaa utaratibu wa kuchukua fedha benki

SEHEMU YA SITA
6.0      VIKAO VYA CHAMA
     6.1       Kamati kuu
6.1.1     Wajumbe wa kamati kuu
                  Viongozi wote  waliopitishwa  na mkutano mkuu wa Afrika Mashariki.
6.1.2  Akidi: Nusu ya wajumbe wote
     
     6.2         Kazi za kamati kuu
6.2.1   Kutafuta vyanzo vya mapato
6.2.2  Kutengeneza na kuratibu sera za Chama
6.2.3  Kuandaa programu ya shughuli za Chama
6.2.4  Kuangalia maendeleo ya   Chama
6.2.5  Kusimamia shughuli za Chama
6.2.6  Kutoa mapendekezo ya Chama na kusimamia utekelezaji  wake
6.2.7  Kuunda kamati mbalimbali za utendaji kutegemeana na uhitaji
6.2.8  Kusimamia ajenda za Mkutano  Mkuu
      Idadi ya vikao vya kamati kuu vitafanyika mara mbili kwa mwaka. Aidha
  Vikao vya dharura vitakuwepo endapo vitahitajika.

6.3          Kamati ya utendaji
Kamati itakuwa na vikao viwili kwa mwaka
                    Kamati ya utendaji itajumuisha Mwenyekiti, Makamu mwenyekiti ,Katibu,
Naibu katibu, Mhazini, Mhazini Msaidizi wa kanda, na Wenyeviti wote wa
Matawi.

6.4  Kamati ya Nidhamu na Usimamizi ya kanda
                                   .
              Itafanya vikao vyake kulingana na majukumu ya wakati husika.
6.4         Mkutano Mkuu wa Chama
6.4.1  Wajumbe wa mkutano Mkuu
                Ni wanaChama wote
6.4.2      Akidi theluthi moja (1/3) ya wanaChama wote
6.4.3       Kazi za Mkutano Mkuu wa kanda.
          Kupitisha mapendekezo ya kamati
          Kupokea taarifa ya kamati
          Kutoa ushauri katika uendeshaji wa Chama
6.5    Idadi ya vikao vya Mkutano Mkuu.
         Mkutano Mkuu utafanyika mara moja kwa mwaka na vikao vya
dharuravitafanyika iwapo vitahitajika. Mkutano mkuu wa Afrika Mashariki
utaambatana na kongamano la Afrika Mashariki.


CHANZO: CHAWAKAMA MUM
Sambaza hii :

1 maoni:

Unknown alisema ...

Nisaidieni namna ya kujiunga ndugu zangu

Tafuta Kwenye Wikipedia

Matokeo ya utafutaji

 
Kwa Hisani ya : Muunda Blogu | Nawaje Ali | NAM
Fahari kwa Kiswahili Jukwaani
Hakimiliki © 2013 - 2018. Kiswahili Jukwaani - Haki Zote Zimehifadhiwa