Matini Muhimu :
Home » » SIKU NIKIFANIKIWA

SIKU NIKIFANIKIWA

Imeandikwa na; Unknown mnamo, Ijumaa, 17 Januari 2014 | Ijumaa, Januari 17, 2014


SIKU NIKIFANIKIWA

Siku nikifanikiwa, swali hili nitatiza
Kweli nitashukuriwa, na watu wasojiweza
Yatima walofiliwa, nitawapa mwangaza
Au taharibikiwa, kwa kuanza kujikweza

Watu nitawaibia, nifanikiwe kwa shari
Dhulma tawafanyia, kwa jeuri na kiburi
Uchawi nitatumia, urozi tangu dahari
Freemason taingia, nikawe hata kafiri

Au nitashughulika, fanikiwe kwa halali
Maharage taridhika, mchunga huku ugali
Ninazoa takataka, kazi yangu ni dhalili
Koradhi kusulubika, kipato kiwe halali

Nitawapa sikitiko, ndugu pia Marafiki
Tulogombea makoko, kipindi nanuka dhiki
Kutokumbuka miiko, kuwaona watubaki
Mbekenyera Kirinjiko, tulisoma kwa hilaki

Nitaheshimu wazazi, au nitawadharau
Nitakumbuka malezi, au nitayasahau
Nitamfata Mwenyezi, diniye chake kirau
Nitakuwa sijiwezi, kwa anasa na vidau

Nitafanya ihsani, au tatenda machafu
Nitakuwa kama nani, lingana wake wasifu
Nami hapa duniani, nitakuwa maarufu
Maswali mengi kichwani, fikira zangu kifipo

Tamati nimefikia, ila jibu sijatoa
Kazi ninawapatia, Islam lobakia
Mdabiri na kujua, kisha mtaniambia

Tahadhari ninatoa, nafsi kujitambua

Chanzo Annur
Sambaza hii :

0 maoni:

Tafuta Kwenye Wikipedia

Matokeo ya utafutaji

 
Kwa Hisani ya : Muunda Blogu | Nawaje Ali | NAM
Fahari kwa Kiswahili Jukwaani
Hakimiliki © 2013 - 2018. Kiswahili Jukwaani - Haki Zote Zimehifadhiwa