FITINA ni nguo mbovu ukiivaa hujastirika!
HUSDA ni mti mkavu ukiukwea utang'oka!
DHARAU ni kiti kibovu ukikalia kitavunjika!
UONGO ni ulemavu si rahisi kuondoka!
UFISADI ni nyumba mbovu tena aishiyo nyoka!
USHIRIKINA ni uovu kwa Mola hutosameheka!
UVIVU ni uonevu katu hutofurahika!
KISWAHILI si hesabu naamini ujumbe umefika!
0 maoni:
Chapisha Maoni